Zaidi ya watu 820 wamekufa, baada ya kutokea tetemeko la
ardhi lenye nguvu katika eneo la kati nchini Morocco, Wizara ya Mambo ya Ndani
ya nchi hiyo imesema.
Tetemeko hilo lenye kipimo cha ukubwa wa alama 6.8, liliibua
hali ya taharuki na kusababisha watu kukimbia katika mitaa ya Jiji la Marrakesh
na katika miji mingine.
Vingi vya vifo hivyo vimetokea kwenye maeneo magumu kufikika
ya mlimani, ambapo pia watu wengine wapatao 153 wamejeruhiwa.
Tetemeko hilo limetokea umbali wa kina cha kilomita 71,
kusini magharibi mwa Marrakesh, kwa muijibu wa ripoti ya wanajiolojia.
0 Maoni