Rais Kagame wa Rwanda kuwania urais kwa muhula wa nne

 

Rais Paul Kagame wa Rwanda, amethibitisha kuwania urais kwa muhula wanne mwakani, jambo litakalomfanya kukaa madarakani kwa karibu miungo mitatu.

"Nina furahishwa na imani waliyonayo kwangu raia wa Rwanda,” Rais Kagame ameliambia jarida la lugha ya kifaransa la Jeune Afrique, jumanne.

Mwezi Machi, Serikali ya Rwanda iliamua kuunganisha tarehe za uchaguzi wa wabunge na wa rais kuwa siku moja, ambao unatarajiwa kufanyika mwezi Agosti mwakani.

Kagame (65), aliingia madarakani mwaka 2000 kupitia kikundi cha wapiganaji wa Rwandan Patriotic Front, kilichowaondoa Wahutu wenye misimamo mikali waliosababisha mauaji ya kimbari.

Chapisha Maoni

0 Maoni