Nchi za Afrika Mashariki, Africa Heritage Fund Kushirikiana UNESCO

 

Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii, Dkt. Hassan Abbasi, akiwa nchini Saudia Arabia katika Mkutano wa 45 wa Kamati ya Urithi wa Dunia leo Septemba 13, 2023, amepata fursa ya kuongoza majadiliano kati ya Tanzania na Uganda.

Majadiliano hayo yanahusu juu ya kushirikiana katika kuainisha na kutangaza maeneo yenye michoro ya miambani iliyopo ukanda wa Ziwa Victoria kwa nchi za Uganda, Tanzania na Kenya ili kuyaingiza kwa pamoja katika Orodha ya Urithi wa Dunia ya UNESCO.

Kufuatia mazungumzo hayo Katibu Mkuu ameelekeza watalaam wa Idara ya Mambo ya Kale nchini waharakishe zoezi la kuainisha maeneo hayo ya Malikale upande wa Tanzania ili yatangazwe na amewashukuru maafisa wa Africa World Heritage Fund ambao wameeleza kusaidia nchi hizo tatu kufanikisha azma hiyo.

Chapisha Maoni

0 Maoni