Mji washangazwa kusambazwa picha za watoto wao waliouchi

 

Wakazi wa mji wenye utulivu kusini mwa Hispania wameshangazwa na kuibuka kwa picha za uchi za watoto wa kike, zinazotengenezwa kwa kutumia teknolojia ya akili bandia (AI) na kusambazwa kwenye mitandao ya kijamii.

Picha hizo za utupu zimekuwa zikitengenezwa zikiwalenga wasichana ambao picha zao za awali walikuwa wamevaa nguo, na nyingi ya picha hizo zilizobadilishwa kwa kutumia teknolojia hiyo ya AI zimetolewa kwenye akaunti zao za mitandao ya kijamii.

Picha hizo huchakatwa kwa kutumia app ya kutengeneza umbo la mtu mhusika bila ya kuwa na nguo, na kisha kusambazwa kwa nia ya kuwadhalilisha na inasadikiwa kuwapo tukio la mmoja wapo kudaia atoa pesa ili picha yake isisambazwe.

Tayari watoto wa kike wapatao 20, wenye umri wa kuanzia miaka 11 na 17 wamejitokeza kulalamikia kufanyiwa kitendo hicho cha matumizi mabaya ya app hiyo, huko Almendralejo, kusini mashariki mwa mkoa wa Badajoz.

Polisi nchini Hispania wanachunguza taarifa hizo, ambapo wavulana 11 wamebainika kuhusika katika kutengeneza picha hizo za utupu ama kusambaza picha hizo kwenye mitandao ya kijamii ya WhatsApp na Telegram.

CHANZO: BBC 

Chapisha Maoni

0 Maoni