Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa ameshiriki sherehe za
uapisho za Rais mteule wa Zimbabwe Mheshimiwa Emmerson Mnangagwa zilizofanyika
katika uwanja wa Harare, Zimbabwe.
Mheshimiwa Rais Mteule Mnangagwa ameshinda uchaguzi huo kwa
kura zaidi ya milioni 2.3 kati ya kura milioni 4.4 zilizopigwa sawa na asilimia
52.6 dhidi ya mpinzani wake Nelson Chamisa ambaye alipata kura milioni 1.9 sawa
na asilimia 44.
Ushindi huo unamfanya Mheshimiwa Mnangagwa kuongoza nchi
hiyo kwa kipindi cha pili cha miaka mitano.
Mheshimiwa Majaliwa amemuwakilisha Mheshimiwa Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan katika uapisho huo
uliofanyika jana.
Rais wa Zimbabwe Mheshimiwa Emmerson Mnangagwa akiwa na mkewe katika sherehe za kuapishwa kwake zilizofanyika jana katika uwanja wa Harare, Zimbabwe.
0 Maoni