Kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong Un anapanga kwenda
Urusi mwezi huu kukutana na Rais Vladimir Putin, afisa mmoja wa Marekani
amesema.
Viongozi hao wawili wanatarajiwa kujadili kuhusu Korea
Kaskazini kuipatia silaha Urusi kuiunga mkono katika vita yake na Ukraine.
Hata hivyo, haijajulikana dhahiri viongozi hao watakutana
katika eneo gani. Pia, si Urusi ama Korea Kaskazini zilizothibitisha taarifa
hizo, zilizoripotiwa pia na vyombo vya habari vya Marekani.
0 Maoni