Maelfu ya watu wanahofiwa kufa baada ya mvua kubwa iliyoambatana
na kimbunga kusababisha mafuriko nchini Libya.
Kiongozi wa serikali ya Libya ya mashariki, ambayo
haitambuliki kimataifa, amesema watu waliokufa wanazidi 2000, na maelfu
hawajulikani walipo.
Mtaalam wa Libya Jalel Harchaoui, ameliambia shirika la
habari la BBC kwamba vifo vilivyotokea vinaweza kufikia maelfu ya watu.
Kimbunga Daniel kiliikumba Libya Jumapili, na kupelekea mamlaka
za nchi hiyo kutangaza kuchukuliwa hali ya juu ya dharura.
0 Maoni