Kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong Un na Rais Vladimir
Putin wamekutana huko Voctochny eneo la mashariki mwa Urusi.
Kim amemuambia Putin kwamba atamuunga mkono daima na kwa
pamoja watapambana na ubeberu.
Kwa upande wake Putin amesema kwamba Urusi itaisaidia Korea Kaskazini
kujenga satelaiti, baada ya taifa hilo kushindwa mara mbili mwaka huu kurusha satelaiti.
Inahofiwa kuwa viongozi hao wawili pia wanaweza
wakakamilisha makubaliano ya kuisaidia silaha Urusi iliyoivamia Ukraine.
Alipoulizwa kuhusina na makubaliano ya masuala ya kijeshi,
Rais Putin alisema kwamba watajadiliana kuhusina na suala hilo.
Kabla ya mkutano wao huo, Korea Kaskazini ilirusha makombora
mawili, ikiwa ni mara ya kwanza kufanya hivyo wakati Kim akiwa nje ya nchi.
0 Maoni