Waokoaji wanahaha kutafuta manusura kwenye vifusi baada ya
tetemeko kubwa la ardhi lililoua watu zaidi ya 2000 nchini Morocco.
Katika eneo lililoathirika mno na tetemeko hilo la ardhi ni
maene0 ya ndani ya mkoa wenye milima kusini-magharibi mwa Marrakesh, ambapo
kijiji kizima nyumba zake zimeanguka.
Mwandishi wa kujitegemea wa BBC Nick Beake amefika katika
moja ya kijiji, walichomkuta mwanamke mzee akipunga mkono kuomba msaada, baada ya
miili ya watu 18 kupatikana.
Waokoaji wanahangaika kufikia maeneo ya ndani zaidi, huku
nyingi ya barabara za mlimani zikiwa zimeharibika.
Kutokana na kuhofia kujirudia kwa tetemeko, wengi wa
wananchi wa Morocco, wameamua kulala nje kwa usiku wa pili, wakilala mitaani.
0 Maoni