Kamati ya siasa wilayani Kwimba mkoani Mwanza imeipongeza
serikali kwa ujenzi wa miradi ya maendeleo katika wilaya hiyo na kusema
itahakikisha inakaba kila eneo kuhakikisha wananchi wanapata huduma kama
walivyowaahidi kwenye Ilani ya Chama cha
Mapinduzi CCM
Kamati hiyo ya wilaya ya Kwimba ikiongozwa na mwenyekiti
wake Sabana Salinja imefika katika shule mpya ya msingi Mwalulyeho na
kuridhishwa na ujenzi wake, na kuipongeza Serikali kwa kuwapunguzia wanafunzi
adha ya kutembea umbali mrefu wa zaidi ya kilometa nane Kwenda katika shule ya
msingi Chalasalawe
“Mimi Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi tupo hapa kwa ajili
ya kuwatembelea na kukagua haya majengo mazuri mazuri yote yanayojengwa na CCM inachoongozwa
na Rais Samia manmjua Rais Samia? Ndiyo huyu anayesababisha msome vizuri
endeleeni kusoma mfike mbali baadae muwe mwenyekiti kama mimi,” amesema Sabana
Salinja.
Akiwa ameongozana na Kamati hiyo ya siasa mkuu wa wilaya ya
Kwimba Ng’wilabuzu Ludigija amesema ataendelea kusimamia miradi ya maendeleo
kama ilani ya chama cha maoinduzi inavyoelekeza na kuwataka wanafunzi wa shule
hiyo kusoma kwa bidii
“Zamani mlikuwa mnasomea Chasalawe mbali kutoka hapa lakini
mmeletewa shule karibu ili msome vizuri sasa nawaomba muitunze vizuri na msome
kwa bidi”.
Mohamed Felician na Mboje Kasomi ni wanafunzi wa shule hiyo
wamempongeza Rais Samia kwa kuwajengea shule hiyo ambayo imewasaidia
kuwapaunguzia kutembea umbali mrefu
“Tunamshukuru Rais Samia kwa kutujengea shule katika Kijiji
chetu hapo mwanzo tulikuwa tunatembea umbali mrefu kwenda katika shule ya Chasalawe
tulikuwa tunachoka sana lakini sasa tunasomea hapa hapa Kijijini kwetu ni
karibu sana tunamuahidi Rais tutasoma kwa bidi na kufaulu” alisema mwanafunzi
huyo.
Mimi online Tv
0 Maoni