Wakulima Katunguru kunufaika na mradi wa umwagiliaji

 

Zaidi ya wakulima 600 wa kata ya Katunguru wilayani Sengerema mkoani Mwanza wanatarajia kunufaika na mradi wa umwagiliaji unaotarajiwa kukamilika mwezi Julai 2024 kwa gharama ya zaidi ya shilingi milioni nne

Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmshauri ya Sengerema Mwita Waryuba akiwa na timu ya watalaamu wa halamashauri hiyo amewataka wasimamizi wa mradi huo kuhakikisha wanashirikiana na jamii katika kutoa elimu ya uhamasishaji wa mradi huo

“Mradi huu umeanza lakini hautakuwa na maana kama mtashindwa kushirikiana na jamii inayowazunguka kwa kurudisha sehemu ya mnachokipata kwa kuwezesha baadhi ya miradi kijijini hapa,” alisema Waryuba.

Kwa upande wake Meneja mradi huo Ombeni Ikola amewataka wananchi hasa wafugaji wanaoishi kuzunguka eneo la mradi huo kutoingiza mifugo kwenye eneo la mradi huo ili mradi ukamilike kwa wakati

Naye diwani wa kata ya Katunguru Sadick Jimola amemuomba meneja mradi kuhakikisha taarifa za mradi zinawafikia wananchi ili kujua kinachoendelea pamoja na kuzingatia kuungana na jamii kwenye masuala ya uwajibikaji kwa jamii.

Mimi Online Tv

Chapisha Maoni

0 Maoni