Ufaransa kutumia dola milioni 171 kuteketeza wine ya ziada

 

Serikali ya Ufaransa imetenga kiasi cha dola za Marekani milioni 171.6 kuteketeza mvinyo wa ziada (wine) pamoja na kuwasaidia wazalishaji wa mvinyo nchini humo.

Hatua hiyo inakuja kufuatia matatizo yanayoikabili sekta ya mvinyo, yakiwamo ya kushuka kwa mahitaji ya mvinyo, kutokana na watu wengi kupendelea kunywa bia.

Uzalishaji mvinyo kwa wingi pamoja na kupanda kwa gharama za maisha pia vinaikabili sekta ya uzalishaji mvinyo nchini Ufaransa.

Idadi kubwa ya fedha iliyotengwa, itatumika kununua mvinyo wa ziada na pombe iliyomo kuuzwa kama bidhaa za vitakasa mikono (sanitizer), bidhaa za kusafishia pamoja na manukato (perfume).

Chapisha Maoni

0 Maoni