Aliyekuwa rais wa Marekani Donald Trump, amejisalimisha
kwenye gereza la wahalifu hatari la Kaunti ya Fulton huko Atlanta, Georgia, na
kuchukuliwa picha kama mhalifu kwa mara ya kwanza.
Trump anakabiliwa na mashtaka 18 yanayohusiana na kula nyama
za kutaka kubadilisha matokeo ya uchaguzi wa rais wa mwaka 2020 katika jimbo la
Georgia.
Trump analazimika kulipa dhamana ya dola laki mbili, ili
kuachiliwa kwenye gereza hilo la Atlanta, wakati akingojea kesi yake kuanza
kusikilizwa.
Hii ni mara ya nne kwa rais huyo wa zamani wa Marekani
kukamatwa ndani ya miezi mitano kwa kesi za uhalifu, ila ni mara ya kwanza kwa
polisi kumpiga picha rasmi kama mtuhumiwa wa uhalifu.
CHANZO: BBC
0 Maoni