Shirikisho la Soka Duniani (FIFA), limeanza mchakato wa kumchukulia
hatua za kinidhamu Rais wa Soka wa Hispania Luis Rubiales kutoka na utovu wa
nidhamu aliouonyesha kwenye fainali ya Kombe la Dunia la Wanawake.
Rais huyo wa Soka wa Hispania Rubiales alifanya kitendo cha
kumbusu mdomoni mchezaji wa timu ya taifa ya wanawake ya Hispania, Jenni Hermoso,
baada ya Hispania kushiinda Uingereza, kwenye mchezo wa fainali.
Kama hiyo haitoshi Rubiales awali alionyesha kitendo kisicho
cha nidhamu cha kushika uume wake huku akishangilia ushindi, baada ya refa
kupuliza kipenga cha kumaliza mchezo huyo wa fainali za Kombe la Dunia la
Wanawake.
Kwa mujibu wa ripoti kutoka Hispania Rubiales anatarajiwa
kutangaza kujiuzulu wadhifa wa Rais wa Soka la Hispania leo Ijumaa, na tayari
ameshawataarifu wenzake katika shirikisho hilo kuhusiana na uamuzi wake huo.
0 Maoni