Serikali ya Somalia yapiga marufuku TikTok na Telegram

 

Serikali ya Somalia imetangaza kupiga marufuku mitandao ya jamii ya TikTok, Telegram pamoja na mchezo wa kubashiri mtandaoni, ikisema mitandao hiyo inatumiwa kusambaza propaganda za magaidi.

Hatua hiyo imekuja, wakati ambapo inajiandaa na awamu ya pili ya oparesheni ya kijeshi dhidi ya kundi la wapiganaji wa Kiislamu wa Al-Shabaab, ambalo limekuwa likifanya mauaji na kukabiliana na serikali kwa miaka 15 sasa.

Katika taarifa hiyo iliyotolewa jana, Wizara ya Teknolojia na Mawasiliano ya Somalia imewaagiza watoa huduma za intaneti kutekeleza katazo hilo ifikapo Agosti 24, la sivyo watakabiliana na hatua za kisheria ambazo hazijaelezwa.

CHANZO: Nation

Chapisha Maoni

0 Maoni