Kapteni wa Hispania Olga Carmon, aliyeifungia nchi yake goli
lililoipa Kombe la Dunia la Wanawake nchi yake, aliambiwa kuwa baba yake
amekufa baada ya mchezo huo.
Carmona, mwenye umri wa miaka 23 alifunga goli pekee dhidi
ya Uingereza katika mchezo wa fainali uliochezwa Jijini Sydney nchini Australia,
na kutwaa kombe hilo.
Baba wa mchezaji huyo anayechezea nafasi ya beki wa kushoto
kwenye timu ya Real Madrid, alikuwa anaugua kwa muda mrefu na alifariki dunia
siku ya Ijumaa.
0 Maoni