Rais Samia Suluhu Hassan, amempa cheti cha hadhi maalum staa wa filamu kutoka nchini China, Jing Dong, kuwa Balozi wa Heshima wa Utalii ili kusaidia kuitangaza Tanzania katika Taifa hilo lenye watu takribani Bilioni 1.4, huku Wachina takribani milioni 200 wakisafiri kwenda kutalii sehemu mbalimbali duniani kila mwaka.
Taarifa iliyotolewa na Ikulu jana jioni kutoka jijini Arusha
ambako Mhe. Rais Samia yupo kwa majukumu mbalimbali ya Kiserikali, imesema Bw.
Jing Dong amepokea heshima hiyo alipokutana na Rais kwa mazungumzo katika kikao
kilichohudhuriwa pia na Waziri wa Utalii, Mohammed Mchengerwa.
Viongozi wengine waliohudhuria tukio hilo kwenye Hifadhi ya
Taifa ya Arusha (ANAPA) ni Katibu Mkuu Dkt. Hassan Abbasi, Mwenyekiti wa
Tanapa, Jenerali Mstaafu George Waitara, Mwenyekiti wa Bodi ya TTB, Balozi Dkt.
Ramadhan Dau na watendaji wengine waandamizi.
Kwa mujibu wa Jarida la Forbes, Bw. Jing Dong ni miongoni
mwa madtaa 100 nchini China, akiwa na wafuasi zaidi ya milioni 200, tuzo zaidi
ya 10 zikiwemo za China Golden Lion Award for Drama (2012) ambayo ni tuzo ya
juu kuliko zote katika eneo la tamthilia za kwenye TV na Msanii Bora wa Kiume
wa China na Msanii Bora wa Televisheni (kupitia filamu za Surgeons na The First
Half of My Life ambazo pia ziliongoza kwa mauzo nchini humo na kuwa maarufu
sana miongoni mwa Wachina).
Mwaka 2018 alishinda Tuzo iliyowashindanisha mastaa wa China
walioko China na Marekani na kushinda kuwa Msanii Bora wa Kiume (Chinese
American Film Festival: Best Actor kupitia filamu ya Mr. Right) na anatajwa
kuwa mmoja wa wasanii wa China maarufu na mabilionea kutokana na kazi yao hiyo.
Baadhi ya filamu na tamthilia zake mashuhuri ni: Nirvana in
Fire (2015), “Ode to Joy” (2016), “Candle in the Tomb” (2016-2017), “Surgeons”
(2017), “Mr. Right” (2018), The People's Property (2019), If Time Flows Back
(2019) and The Best Partner (2020).
Nyingine ni: Legend of Entrepreneurship (2012), The
Disguiser (2015), Candle in the Tomb (2016), Surgeons (2017) and The First Half
of My Life (2017).
0 Maoni