James Harden amepigwa faini ya dola 100,000 na NBA kwa
kusema kuwa hatoichezea Philadelphia76ers, iwapo rais Daryl Morey ataendelea
kuwapo madarakani.
Mchezaji huyo wa ligi ya NBA, alimuita Morey “muongo” kwenye
mahojiano baada ya ripoti kuwa 76ers imesitisha mazungumzo ya kumuuza.
Harden, mwenye umri wa miaka 33, aliripotiwa kutamani
kujiunga na timu ya LA Clippers kabla ya mazungumzo ya mpango huo kuzimwa.
NBA imesema kuwa faini hiyo ni kwa kusema hatotekeleza
majukumu yake ya kuichezea timu hiyo iwapo hatouzwa timu nyingine kinyume na
mkataba wake wa kazi.
0 Maoni