Kapteni wa England Harry Kane, amefunga na kutengeneza goli
katika mchezo wake wa kwanza Bundesliga wakati mabingwa Bayern Munich wakishinda
magoli 4-0 dhidi ya Werder Bremen.
Kane alitupia goli hilo wavuni kwa mpira wa chini wa shuti
la guu la kulia uliompita kipa Jiri Pavlenka na kuifanya Bayern kuongoza kwa magoli
mawili.
Awali Kane alitoa pande la goli lililofungwa na Leroy Sane
ambaye katika mchezo huo aliifungia Bayern Munich magoli mawili.
Mchezaji Mathys Tel alikamilisha ushindi huo murua kwa kocha
Thomas Tuchel katika dakika za mwishoni.
0 Maoni