DC Kwimba awataka wanafunzi waliofaulu kidato cha tano kuripoti shuleni

 

Mkuu wa wilaya ya Kwimba, Bw. Ng’wilabuzu Ludigija, amewataka wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na shule za sekondari zilizopo katika wilaya hiyo kuripoti katika shule zao, ili waanze kupata elimu baada ya serikali kukamilisha ujenzi wa maiundombinu ya madarasa, vyoo na mabweni.

Bw. Ludigija amesema nafasi zao zipo na kama kuna wengine wanataka kuhamia katika shule hizo za Mwamashimba, Sumve, Talo na Ngudu wanakaribishwa huku akimshukuru Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha za kuboresha na kujenga miundombinu katika shule hizo ili wanafunzi wapate mazingira mazuri ya kujisomea.

Mkuu wa wilaya huyo amesema tangu shule zilipofunguliwa hadi leo hii wanafunzi wanaendelea kuripoti na kwamba ataendelea kutembelea shule hizo ili kuhakikisha wanafunzi wote wanaripoti na kuanaza masomo yao.

“Naendelea kusema kwa wananchi hasa wazazi waendelee kuwaleta shuleni watoto wao, na shule zote za kidato cha tano tumejipanga kwa miundombinu ya kutosha waje tu hapa tunawasubiri na vitanda vipo vya kutosha hadi vinabaki, Rais Samia amefanya mapinduzi makubwa sana kwenye miundombinu ya kujifunzia pamoja na madarasa na shule za kwimba ni moja kati ya shule zinanofanya vizuri sana,” alisema Bw. Ludigija.

Kwa upande wao wanafunzi wa shule ya sekondari Mwamashimba akiwemo Hamisa Saidi na Ana Ayoub, wamemuahidi mkuu huyo wa wilaya kufanya vizuri katika masomo yao ili warudishe fadhila kwa Rais Samia Suluhu Haasan kwa jinsi alivyowawekea mazingira mazuri ya kujisomea.

“‘Tunapenda kumshikuru sana Rais Samia kwa kutusaidia tulipofika hapa shuleni tukaona madarasa mabweni na vyoo vizuri tunamuahidi kufaulu vizuri sana na tutapata division one nyingi sana tunamshukuru sana,” walisema wanafunzi hao.

Baadhi ya wanafunzi wa kidato cha tano waliochaguliwa kujiunga na shule za sekondari zilizopo katika wilaya ya Kwimba Jijini Mwanza wakiwasili shuleni na mizigo yao tayari wa ajili ya kuanza masomo yao rasmi.


Mkuu wa wilaya ya Kwimba, Bw. Ng’wilabuzu Ludigija, aliyevaa fulana ya bluu akikagua miundombinu ya shule iliyojengwa na serikali ili kuboresha mazingira ya kusomea kwa wanafunzi wanaojiunga na kidato cha tano.


Chapisha Maoni

0 Maoni