Mmoja wa miongoni mwa walioshiriki kuchanganya udongo wa
iliyokuwa Tanganyika na Zanzibar, Bi. Khadija Abbas Rashid, 74, amefariki dunia
jana Agosti 22, 2023 nyumbani kwake Rahaleo Mkoa wa Mjini Magharibi.
Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano, imethibitisha taarifa za kutokea
kwa kifo cha Bi. Khadija Abbas Rashid, kupitia taarifa yao waliyoisambaza kupitia
kwenye mitandao mbalimbali ya kijamii leo Agosti 23, 2023
Marehemu Bi. Khadija Abbas Rashid alihusika katika tukio hilo la kuchanganya udongo wa Tanganyika na Zanzibar Aprili 26, 1964.
0 Maoni