Ajabu miili mipya ya waumini wanaokufa kwa njaa yazikwa Shakahola

 

Huenda baadhi ya wasaidizi wa kiongozi wa dhehebu tata la Kilifi huko Kenya, Paul Mackenzie, bado hawajakamatwa baada ya kubainika kwa miili mingine mipya ya watu iliyozikwa kwenye eneo la kanisa hilo la msitu wa Shakahola.

Miili kadhaa ya watu imefukuliwa katika msitu huo wa Shakahola wiki hii, ambapo inaonyesha dhahiri maiti za watu hao zimezikwa katika siku za hivi karibuni, baada ya kufunga hadi kufa.

Chanzo kimoja kutoka kwa timu inayofukua miili ya waumini wa kanisa hilo tata, amesema miili hiyo imezikwa muda wa mwezi mmoja uliopita, wakati timu inayofukua miili ilipopumzika zoezi hilo kwa wiki mbili.

Makaburi hayo ya watu yalionekana kuwa ni mafupi na yamefukiwa kwa juu juu, hali inayoashiria kwamba bado kuna wasaidizi wa kiongozi wa kanisa hilo, wanaoendeleza imani potofu ya waumini kufuanga hadi kufa ili kukutana na Mungu.

Siku ya jumanne, timu ya wafukuaji makaburi ya waumini waliozikwa msitu wa Shakahola imefanikiwa kufukua miili 16, ikiwamo baadhi ya miili ya watu ambayo inaonekana imezikwa katika siku za karibu.

Chanzo: Nation


Chapisha Maoni

0 Maoni