Wakili Harold Sungusia amechaguliwa kuchaguliwa kuwa Raisi wa Tanganyika Law Society (TLS) akirithi mikoba ya Prof Edward Hoseah ambaye amemaliza muda wake.
Sungusia ametangazwa mshindi kwa mwaka 2023-2024 kwa kupata kura 748 kati ya kura 825 huku Aisha Sinda akichaguliwa kuwa Makamu wa Raisi wa Tanganyika Law Society kwa mwaka 2023-2024 kwa kupata kura 527 kati ya kura 825.
Kwa upande wa mwekahazina nafasi imechukuliwa na Wakili Christopher Alex kwa kupata kura 807 Kati ya Kura 825
Pia wakili Edward Heche amechaguliwa kwa kuwa Mwenyekiti wa Umoja wa Mawakili Vijana(AYL) wa TLS kwa mwaka 2023-2024
Prof Hoseah atakabidhi kijiti rasmi baada ya kuitumikia TLS Kuanzia mwaka 2021 pia aliwahi kuwa Mkurugenzi wa Taasisi ya kuzuia na kupambana Rushwa (TAKUKURU) nchini Tanzania.
0 Maoni