Rais William Ruto na mpinzani wake mkuu Raila Odinga
wamepeana mikono kwa mara ya kwanza tangu kumalizika kwa uchaguzi mkuu Agosti nwaka
2022.
Raila ambaye waziri mkuu mstaafu amekutana na Rais Ruto muda
huu ambapo wawili hao wanahudhurika kwenye maziko ya shujaa wa vita ya Mau Mau
Mukami Kamathi.
Kitendo hicho cha wanasiasa hao kusalimiana hadharani kwa
mara ya kwanza kilimevutia waombolezaji wanaohudhuria maziko hao.
Katika maziko hayo Raila alisalimiana pia na Naibu Rais wa
Kenya Rigathi Gachagua pamoja na Waziri Musalia Mudavadi.
Akiongea kwenye maziko hayo Mbunge wa Naivasha Jayne Kihara
alimuomba Raila Odinga kuacha maandamano ili serikali ifanyekazi.
"Raila nakuomba uwache serikali ifanye kazi, usirudi
kwa barabara," alisema mbunge huyo.
0 Maoni