Rais Samia katika ukurasa wake kwenye mtandao wa twita ameandika “Nimepokea kwa masikitiko taarifa za kifo cha Ndugu Bernard Membe”
Rais Samia amesema Kwa zaidi ya miaka 40, Ndugu Membe alikuwa mtumishi mahiri wa umma, mwanadiplomasia, Mbunge na Waziri aliyeitumikia nchi kwa weledi. “Pole kwa familia, ndugu, jamaa & marafiki. Mungu amweke mahali pema. Amina.”
Membe alizaliwa Novemba 9 1953 alishika kushika nyadhifa mbalimbali serikalini na mwaka 2020 aliwania urais kupitia Chama cha ACT Wazalendo baada ya kutimuliwa CCM wakati wa utawala wa hayati John Magufuli na kurejea tena katika utawala wa serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Dk Samia Suluhu Hassan.
0 Maoni