Picha ya kwanza yenye uhalisia ya meli Titanic yapigwa

 


Mabaki ya moja ya meli maarufu duniani ya Titanic yamebainika vyema kwa mara ya kwanza tangu meli hiyo izame miaka 111 iliyopita.

Picha kamili ya digitali ya Titanic, ambayo imezama chini baharini mita 3,800 katika eneo la Atlantic, imepiigwa kupitia vipimo vya kina kirefu.

Picha hiyo ya teknolojia ya 3D inaonyesha meli hiyo yote, kwa muonekano wa kama vile maji yameondolewa.

Ni matumaini sasa itawezekana kupata jawabu la nini haswa kilitokea kwenye meli hiyo kubwa wakati ilipozama mnamo mwaka 1912.

Watu zaidi ya 1,500 walikufa wakati meli hiyo ilipogonga pande la barafu ikiwa katika safari yake ya  kutoka mji wa Southampton, England hadi New York, Marekani.



Chapisha Maoni

0 Maoni