Mkulima anayefuga mamba, ameshambuliwa na mamba wake
kaskazini mwa Cambodia na mwili wake kuchanwa chanwa vipande na mamba wapatao
40, baada ya kuanguka kwenye banda lao.
Mkulima huyo Luan Nam, 72, alikuwa anajaribu kutoa kwenye
banda yai lililokuwa limelaliwa na mamba, ndipo myama huyo alipoing’ata fimbo
yake na kumvuta bandani.
Mkuu wa Jeshi la Polisi, Mey Savry, amesema baada ya kudondoka
bandani, mkulima huyo aliaanza kushambuliwa na mamba wengine aliokuwa anawafuga.
Savry ameliambia shirika la habari la AFP news, kwamba tukio
hilo limetokea katika mji wa Siem Reap siku ya jana Ijumaa.
Mwili wa mkulima Nam ambaye alikuwa ni rais wa chama cha wafugaji
wa mamba Cambodia, ulitolewa ukiwa na alama za kung’atwa, ambapo mkono wake
mmoja haukupatikana.
0 Maoni