Na.
Beda Msimbe (TBN) Petersburg, Urusi
BODI ya Utalii Tanzania
(TTB) inajipanga kumega keki ya utalii inayotengenezwa na Urusi kwa
lengo la kulipatia taifa zaidi ya dola za Marekani 500 kwa mwaka.
Zaidi ya wananchi milioni 13.4 wa Urusi hutalii sehemu mbalimbali
duniani na kutokana na kuwa watumiaji wazuri wa vipato vyao, Tanzania
ikipata angalau asilimia 1 ya watu hao ambacho ni sawa na watu
134,000 ambao wataingiza dola milioni 500.
Kauli hiyo
imetolewa na Mkurugenzi Mkuu wa TTB, Ephraim Mafuru katika Jukwaa la
Kimataifa la Uchumi la Petersburg (SPIEF’26) linaloendelea mjini
hapa.
Mafuru alisema katika mikakati hiyo wanataka katika
miaka 10 ijayo kufikisha watalii mara mbili ya hao na hivyo
kuliingizia pato taifa la dola za Marekani bilioni moja.
Akiwa
katika banda la Tanzania katika jukwaa hilo alisema anafurahi kwa
Rais Samia kuendelea kuelekeza maono kwa vitendo katika kusaka
wawekezaji.
Pia
kufungua fursa za Watanzania kwa ziara zinazojumuisha watendaji
wakuu wa maeneo muhimu ya taifa kama miundombinu, utalii na madini
ili diplomasia ya uchumi iwe na maana kwa taifa.
Mafuru
amesema kama nchi wamedhamiria kuhakikisha wanafungua soko la Urusi
kwani katika utamaduni wa utalii, wanaongoza duniani na wanaongoza
pia kwa matumizi ya kifahari (anasa).
Alisema wamekuwa na
mikutano mingi ya utafiti na kubaini watalii hao walikuwa wanashindwa
kufika kutokana na umbali lakini kuanza kwa safari za Ndege za ATC za
moja kwa moja zitapunguza muda wa kusafiri kwa wananchi hao na kuwa
sehemu ya hamasa ya kuja kutembelea Tanzania.
Aidha alisema
kwamba wakati umefika kwa wananchi wa tanzania kujifunza Kirusi kwa
ajili ya kuvutia watalii ambao hufurahishwa ikiwa wataongozwa kwa
lugha ya nyumbani kwao.
Akizungumzia jukwaa na kongamano
alisema ziara ya Rais Samia nchini Urusi imekuwa na mafanikio makubwa
ambayo yatachangia kukua kwa utalii na pia kusaidia sekta ya
uwezekaji na biashara.

.jpeg)

0 Maoni