Tanzania sasa ina takwimu za maendeleo zinazopimika

 

Mgombea Urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Samia Suluhu Hassan, na chama chake wamefanikiwa kudhihirisha wazi kwamba wanatosha na wameiandaa Tanzania kwa hatua kubwa inayofuata ya maendeleo, huku wakikabiliana na wapotoshaji wachache kwa kutumia lugha moja tu: Matokeo Yanayopimika.

Tukielekea Uchaguzi Mkuu, kuna jambo moja lisilopingika: Ukweli hauwezi kufichwa. Wanaojaribu kufunika jitihada kubwa za maendeleo nchini wamejikuta wakiumia kwa sababu jua la mafanikio linaangaza kila kona ya taifa.

Dkt. Samia alikabidhiwa nchi wakati ikiwa kwenye majonzi, lakini badala ya kutetereka, alisimama imara. Ameiweka Tanzania katika viwango vipya vya uongozi vinavyopimika si kwa maneno matupu, bali kwa takwimu na matokeo yanayoonekana kwa macho.

Mageuzi Makubwa katika Nishati na Elimu

Chini ya uongozi wake, sekta ya Nishati imeshuhudia mabadiliko makubwa. Uzalishaji wa umeme nchini umeongezeka kutoka megawati 1,602 mwaka 2020 hadi kufikia megawati 3,078 mwaka 2024. Ongezeko hili kubwa, ambalo linatokana kwa kiasi kikubwa na mradi wa Bwawa la Mwalimu Julius Nyerere (JNHPP), linatoa uhakika wa umeme wa kutosha kwa viwanda na matumizi ya nyumbani.

Sambamba na hilo, dhamira ya kupeleka umeme hadi vijijini imeimarika, ambapo vijiji vyenye umeme vimeongezeka kutoka 8,587 mwaka 2020 hadi kufikia 12,318 mwaka 2024. Hii ni ishara ya wazi ya kuondoa giza na kupeleka maendeleo kwa wananchi wa hali ya chini.

Katika sekta ya Elimu, namba zinaonesha ari mpya. Idadi ya shule za msingi imeongezeka kutoka 16,656 mwaka 2020 hadi 19,783 mwaka 2024, huku shule za sekondari zikipanda kutoka 5,000 hadi 5,929. Hatua hii inahakikisha watoto wa Kitanzania wanapata nafasi za kutosha za elimu bora kuanzia chini hadi juu.

Afya na Uchumi wa Mwananchi Zaimarishwa

Uboreshaji wa sekta ya Afya pia umekuwa kipaumbele. Upatikanaji wa dawa na vifaa tiba umeimarika kutoka asilimia 75.6% mwaka 2020 hadi asilimia ya kuvutia ya 89.3%, hatua inayoimarisha huduma za afya nchini kote.

Katika kusaidia wananchi wengi, Serikali imewekeza katika sekta za uzalishaji. Matumizi ya mbolea kwenye Kilimo yameongezeka kutoka tani 586,604 mwaka 2020 hadi zaidi ya milioni 1.2 mwaka 2024. Aidha, eneo linalotumia umwagiliaji limepanda kwa kasi kutoka hekta 561,383 hadi 983,466, hatua muhimu ya kuifanya kilimo kisitegemee mvua.

Katika sekta ya Uvuvi, wavuvi wamewezeshwa kwa ongezeko la boti za kisasa kutoka 280 mwaka 2020 hadi 507 mwaka 2024, na hivyo kuongeza tija na kipato chao.

Propaganda Zatafunwa na Ukweli

Haya yote ni ushahidi wa dhahiri kwamba Mama Samia si kiongozi wa maneno, bali wa matokeo ya kweli. Wanaojaribu kupotosha ukweli huu wanapaswa kuelewa kuwa Tanzania ipo kwenye njia ya maendeleo isiyozuilika.

Kazi na utekelezaji vinafanywa kwa vitendo, na jitihada zozote za kutumia propaganda za kisiasa kuzuia safari hii zitakumbana na ukweli wa takwimu hizi. Ukweli unaendelea kuangaza – na ukweli huo ni huu: Mama Samia ameahidi, na ametekeleza.

Chapisha Maoni

0 Maoni