Tunatambua mchango wa NGOs katika maendeleo: RC Lindi

 

Mkuu wa Mkoa wa Lindi Mhe. Zainab Telack amesema Serikali inatambua mchango wa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali katika kuleta maendeleo kwa wananchi.

Hayo yamesemwa mkoani Lindi kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa huo na Mkuu wa Wilaya ya Linda Mhe. Victoria Mwanziva wakati akifungua Jukwaa la Mwaka la Mashirika Yasiyo ya Kiserikali mkoani humo.

Mhe. Victoria amesema Serikali inatambua mchango wa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali kwani ni muhimu katika kuhakikisha mipango ya Serikali inatimia ya kuwahudumia wananchi katika maeneo mbalimbali kupitia sekta mbalimbali zenye kuigusa jamii.

"Niseme kuwa NGOs ni mkono wa pili wa Serikali katika kuleta maendeleo kwa jamii hivyo tutaendelea kuweka mazingira mazuri na wezeshi ya kufanya kazi zenu na kutekeleza miradi mbalimbali." amesema Mhe. Victoria

Ameongeza kuwa Mashirika hayo yanatakiwa kufanya zao kwa kuzingatia Sheria na taratibu zilizopo ikiwemo kutekeleza matwajanya Sheri ya Mashirika Yasiyo ya Kiserikali kwa kuhakikisha wanatoa taarifa zao za robo Mwaka na Mwaka na mikataba ya kifedha katika utekelezaji wa miradi mbalimbali.

"Tufuate Sheria na Kanuni zilizopo katika utekelezaji wa majukumu yetu haswa katika kufanya kazi na Mamlaka ambazo tunafanya kazi zetu mfano Afya, Maji, Elimu, Mazingira na Sekta zingine ili tuwe na uratibu mzuri wa utekelezaji wa miradi," amesisitiza Mhe. Victoria.

Kwa upande wake Mwakilishi wa Msajili wa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali kutoka Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Fransisca Mwendesha amesema Serikali inatambua kazi kubwa ya Mashirika Yasiyo ya Kiserikali katika kuwahudumia wananchi ila ameyataka Mashirika hayo kuendelea kuzingatia Sheria taratibu zilizopo ili waweze kuwa katika mazingira mazuri ya Utekelezaji wa majukumu yao.

Naye Mwenyekiti wa Baraza la Taifa la Mashirika Yasiyo ya Kiserikali (NACoNGO) Jasper Makala amesema Baraza hilo linaendelea kuwa kiungo muhimu katika ya Sekta ya NGOs na Serikali,hivyo amewaomba Mashirika hayo kuendelea kuzingatia Sheria taratibu zilizopo katika utekelezaji wa majukumu ili kutimizaalengo ya Shirika na Serikali kwa ujumla.

Majukwaa ya Mashirika Yasiyo ya Kiserikali kuanzia ngazi ya Halmashauri mikoa na Taifa yanaongozwa na Kaulimbiu isemayo: Tathmini ya Mchango wa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali katika Maendeleo ya Taifa 2020/2021-2024/2025; Mafaniko, Changamoto, Fursa na Matarajio.



Chapisha Maoni

0 Maoni