Mshambuliaji wa Liverpool Jota afariki dunia kwa ajali Hispania

 

Mshambuliaji wa Liverpool, Diogo Jota, amefariki dunia katika ajali ya gari nchini Hispania baada ya gari lake kutoka barabarani kufuatia kupasuka kwa tairi alipokuwa akipita gari jingine, kwa mujibu wa polisi wa eneo hilo.

Ndugu yake, Andre Silva, naye pia alipoteza maisha kwenye ajali hiyo. Jota, mwenye umri wa miaka 28, alifunga ndoa na mchumba wake mwezi uliopita, walikuwa na watoto watatu pamoja.

Mchezaji huyo wa kimataifa wa Ureno alikuwa sehemu muhimu ya kikosi cha Liverpool kilichoshinda Ligi Kuu ya England msimu uliopita.

Timu ya taifa ya Ureno imesema Jota hakuwa tu "mchezaji wa kipekee" bali pia "mtu wa aina yake  aliyekuwa akiheshimika na wachezaji wenzake wote pamoja na wapinzani wake."




Chapisha Maoni

0 Maoni