Viongozi wa dini Muhimbili wamuaga Prof. Janabi na kuliombea taifa amani

 

Viongozi wa dini mbalimbali Hospitali ya Taifa Muhimbili wamekutana na Mkurugenzi mpya wa Shirika la Afya Duniani (WHO) Kanda ya Afrika, Profesa Mohamed Janabi, kwa lengo la kumpongeza, kumuaga rasmi, pamoja na kuliombea taifa la Tanzania amani, mshikamano na uongozi bora.

Viongozi hao kutoka madhehebu ya Kikristo, Kiislamu na mengineyo, wameungana na watumishi wa hospitali hiyo na kuonesha mshikamano wao katika kumuaga Prof. Janabi, ambaye kwa miaka mingi ametoa mchango mkubwa katika sekta ya afya nchini.

Katika hatua nyingine, viongozi hao wa dini wameomba dua na sala kwa ajili ya taifa la Tanzania, wakilitakia amani, umoja na maendeleo endelevu pamoja kumuombea Profesa Janabi baraka na hekima katika majukumu yake mapya.

Profesa Janabi amechaguliwa kuwa Mkurugenzi wa Kanda ya Afrika wa Shirika la Afya Duniani (WHO), Mei 18 mwaka huu na anatarajiwa kuanza kazi rasmi katika makao makuu ya WHO Kanda ya Afrika, yaliyoko Brazzaville, Jamhuri ya Congo, ambapo atakuwa na jukumu la kuratibu na kuongoza sera za afya kwa nchi wanachama wa bara la Afrika.

Chapisha Maoni

0 Maoni