Rais
wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi,
amesema kuwa ushirikiano wa nchi wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa
Afrika (SADC) katika kuimarisha hifadhi zinazovuka mipaka ni nyenzo muhimu ya
kuzifanya kuwa endelevu na zenye manufaa kwa kila nchi.
Rais
Dkt. Mwinyi ameyasema hayo leo tarehe 23 Mei 2025 katika kikao cha Wakuu na
Viongozi wa Serikali wa nchi za SADC kilichofanyika jijini Harare, Zimbabwe,
kilicholenga kujadili uimarishaji wa hifadhi hizo katika ukanda wa SADC, ambapo
amemwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu
Hassan.
Mkutano
huo ni sehemu ya maadhimisho ya
mafanikio ya miaka 25 tangu kuanzishwa kwa mpango wa uhifadhi wa hifadhi
zinazovuka mipaka kikanda.
Rais
Dkt. Mwinyi ameeleza kuwa umefika wakati kwa sera za nchi wanachama kuendana na
sera kuu za SADC katika biashara ya kaboni, pamoja na kubadilishana uzoefu
badala ya kila nchi kuwa na sera tofauti kwa maslahi ya kikanda.
Aidha,
amesema kuwa mkutano huo umeonesha dira na utayari wa SADC katika uhifadhi wa
pamoja wa bahari, wanyamapori, rasilimali za maji, misitu, na kusisitiza zaidi
katika uchumi wa buluu eneo ambalo
Zanzibar inalitegemea kwa kiasi kikubwa.
Vilevile,
Rais Dkt.Mwinyi amesisitiza umuhimu wa kuzishirikisha zaidi jamii, sekta
binafsi, washirika wa maendeleo, wadau na asasi zisizo za kiserikali katika
kufanikisha azma ya pamoja ya uhifadhi.
Halikadhalika
Rais Dkt.Mwinyi ametoa wito kwa nchi wanachama wa SADC kuimarisha ushirikiano
na kubadilishana uzoefu baina yao, kwani uhifadhi wa hifadhi zinazovuka mipaka
unahitaji mshikamano wa kweli na juhudi za pamoja.
Akizungumza
katika mkutano huo, Mwenyekiti wa Jumuiya ya SADC ambaye pia ni Rais wa
Zimbabwe, Mhe. Emmerson Dambudzo Mnangagwa, amesema kuwa kuna umuhimu mkubwa wa
kuwashirikisha wananchi ili nao wawe sehemu ya juhudi za pamoja za kuimarisha
hifadhi zinazovuka mipaka na kuzifanya kuwa endelevu.
0 Maoni