Mhe. Mchengerwa aboresha taarifa zake Daftari la Kudumu la Wapiga kura

 

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais- TAMISEMI, Mhe. Mohamed Mchengerwa ameshiriki  kwenye zoezi la  kuboresha taarifa zake kwenye Daftari la Kudumu la Mpiga Kura Ikwiriri - Rufiji.

Mara baada ya kuboresha taarifa zake jana Mei 20, 2025, Mhe. Mchengerwa amewataka wananchi kote nchini kutumia muda wa siku mbili zilizobaki  kuboresha taarifa zao.

"Naomba kutoa wito kwa wananchi kwenda kuboresha taarifa zao katika kipindi hiki kifupi cha siku mbili ili waweze kupata haki yao ya msingi ya kupiga kura kwa maendeleo ya taifa letu," amesisitiza Mhe Waziri Mchengerwa.

Aidha, amefafanua kuwa zoezi la kuboresha taarifa ni la muhimu kwa kuwa taarifa hizo zinaweza pia kutumika na Serikali ili kuleta maendeleo.

Pia Waziri Mchengerwa ametoa wito kwa watanzania kutumia vizuri hali yao ya kupiga kura wakati utakapofika.




Chapisha Maoni

0 Maoni