Polisi na TAWA wawanasa watu wawili wakiwa na meno ya tembo

 

Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya kwa kushirikianana Askari wa Mamlaka ya Usimamizi Wanyamapori Tanzania (TAWA) linamshikilia Riziki Charles Mapila (55) mkazi wa Lubele Wilaya ya Kyela akiwa na nyara za Serikali vipande tisa vya meno ya tembo bila kibali.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mbeya SACP Benjamin Kuzaga amesema mtuhumiwa alikamatwa Aprili 14, 2025 na Askari waliokuwa doria katika Kitongoji cha Isaki, Kata ya Njisi, Tarafa ya Unyakyusa, Wilaya ya Kyela akiwa na vipande hivyo 9 vya meno ya tembo vyenye uzito wa kilogram 34.6 akiwa amehifadhi ndani ya mfuko wa sandarusi kisha kuficha porini.

Wakati huo huo, Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya kwa kushirikianana Askari wa TAWA Wilaya ya Mbarali linamshikilia Kenedy Yawaga (37) Mkazi wa Itamba akiwa na nyara za Serikali vipande vitatu vya meno ya tembo bila kibali.

Mtuhumiwa alikamatwa Aprili 03, 2025 katika Kijiji cha Mabadaga kilichopo Kata ya Mapogoro, Tarafa ya Rujewa, Wilaya ya Mbarali, Mkoani Mbeya katika oparesheni maalum dhidi ya wahujumu uchumi wa Taifa akiwa na nyara hizo zenye uzito wa kilogram 12 akiwa amefunga kwenye mfuko wa sandarusi na kishakufukia ardhini kwenye shamba lake lililopo kwenye mji wake.

Kamanda Kuzaga amesema kwamba uchunguzi wa awali umebaini kuwa watuhumi wawali kuwa wanajihusisha na uwindajiharamu katika Hifadhi za Taifa, taratibu za kuwafikisha Mahakamani zinaendelea.



Chapisha Maoni

0 Maoni