TMDA yaandaa tuzo kwa Waandishi wa Habari

 

Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba (TMDA) imeandaa tuzo maalum kwa waandishi wa habari ambao wameripoti taarifa na kuandaa makala mbalimbali kuhusu kazi na majukumu ya TMDA katika kipindi cha kuanzia Julai, 2024 hadi Machi 2025.

Taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi Mkuu wa TMDA imesema lengo la tuzo hizo ni kutambua mchango wa waandishi wa habari na kuleta hamasa katika kuelimisha jamii kuhusu masuala ya udhibiti wa dawa, vifaa tiba, vitandanishi na bidhaa za tumbaku kupitia vyombo vya habari ili kulinda afya ya jamii.

Kazi zinazolengwa ni zile zilizoripotiwa kupitia Runinga (TV), Redio, Magazeti na Mitandao ya Jamii kwa kipindi tajwa, ambapo baada ya kupokelewa zitashindanishwa na hatimaye kuwapata washindi watakaopewa tuzo.

TMDA inawaalika waandishi kuwasilisha kazi zao kabla ya kufika tarehe 18 Aprili, 2025 kupitia anuani ya barua pepe ya commpedtmda@gmail.com au kwa njia ya CD katika ofizi za TMDA zilizopo Dodoma, Dar es Salaam, Mwanza, Arusha, Mtwara, Tabora na Geita.

Chapisha Maoni

0 Maoni