Mwenyekiti wa
Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF) Deodatus Balile amechukua fomu ya kuwania
tena nafasi hiyo kwa kipindi cha miaka minne, ikiwa zimebaki siku 15 kabla ya kufanyika
uchaguzi wa viongozi wa TEF.
Balile amechukua
fomu leo tarehe 21 Machi 2025 katika ofisi za TEF zilizopo Kisutu Jijini Dar es
Salaam kutetea nafasi hiyo, huku akisindikizwa na baadhi ya wanachama wa chama
hicho.
Uchaguzi wa
TEF utafanyika tarehe 5 Aprili 2025 Songea mkoani Ruvuma ambapo utatanguliwa na
Mkutano Maalum utakaoanza tarehe 3 Aprili 2025.
Mkutano huo
unatarajiwa kufunguliwa na Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk.
Emmanuel Nchimbi.
Balile
amekuwa Mwenyekiti wa jukwaa hilo baada ya kushinda kwenye uchaguzi uliofanyika
mwaka 2021.
Jumla ya
wagombea 14 tayari wamechukua fomu za kugombea ambapo katika nafasi ya Ujumbe
wa Kamati ya Utendaji ya TEF wamechukua wagombea 12, nafasi ya Makamu
Mwenyekiti na Mwenyekiti zina mgombea mmoja mmoja.
Mwisho wa
kuchukua na kurejesha fomu ni Jumatatu tarehe 24 Machi 2025.


0 Maoni