Machi mosi mwisho wa kutumia tiketi mwendo kasi Dar

 

Wakala wa Mabasi Yaendayo Haraka (DART) imesema kuanzia mwezi Machi mwaka huu wa 2025 itasitisha rasmi matumizi ya tiketi za karatasi katika usafiri wa Mabasi Yaendayo Haraka na badala yake watumiaji wote wa mabasi hayo watatakiwa kutumia kadi janja ambazo zinaendelea kuuzwa katika vituo vikuu vya mradi huo.

Akiongea Jijini Dar es Salaam wakati wa kuhitimisha mradi wa maendelezo yatokanayo na uboreshaji wa usafiri wa umma (TOD), Mtendaji Mkuu wa DART, Dkt. Athumani Kihamia amesema ifikapo Machi mosi matumizi ya tiketi za karatasi katika kulipia nauli za mwendokasi yatasitishwa.

Dkt. Kihamia amesema matumizi ya kadi yanaondoa usumbufu wa kukosekana kwa chenchi lakini pia ni njia muafaka ya kudhibiti uvujaji na upotevu wa mapato ya Serikali.

Chapisha Maoni

0 Maoni