CHADEMA wameamua wamchagua Tundu Lissu

 

Tundu Lissu ametangazwa kuwa mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti wa Taifa wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), katika uchaguzi uliofanyika jana usiku.

Akitangaza matokeo hayo leo na Mwenyekiti wa Uchaguzi Prof. Raymond Mushi amesema, wapigakura waliojisajili walikuwa 1,014 kura zilizopigiwa ni 999, halali zikiwa 996 na tatu zimeharibika.

Prof. Mushi ameeleza kuwa Odero Odero kapata kura moja sawa na asilimia 0.1, Freeman Mbowe amepata kura 482 sawa na asilimia 48.3 huku Lissu akipata kura 513 sawa na asilimia 51.5.

Kwa upande wa Nafasi ya Makamu Wenyekiti wa Chadema Zanzibar ameshinda Said Mzee Said ambaye amepata kura 625 sawa na asilimia 89 ya kura 706 huku kura halali zikiwa 700 na sita zimeharibika.

Chapisha Maoni

0 Maoni