Mwanafunzi UDOM afa maji maporomoko ya Sanje

 

Jeshi la Polisi Mkoa wa Morogoro linachunguza kifo cha mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM), ambaye amekufa maji kwenye maporomoko ya maji ya Sanje yaliyo katika Hifadhi ya Taifa ya Udzungwa Wilaya ya Kilombero Mkoa wa Morogoro.

Tukio hilo limetokea jana Desemba 22, 2024 majira ya mchana ambapo mwanafunzi wa mwaka wa kwanza wa UDOM Hezekiel Petro (21) anayesoma masomo ya sanaa na historia alikufa maji baada ya kukanyaga jiwe lenye utelezi na kutumbukia kwenye kina kirefu cha maji.

Mwanafunzi huyo alifika katika maeneo hayo akiwa kwenye ziara ya mafunzo kwa vitendo na wanafunzi wenzake zaidi ya 300 wakiwa wamefuatana na wakufunzi wao ambapo mwili wa mwanafunzi huyo ulitolewa kwenye maji na wataalamu wa kuogelea.

Kufuatia tukio hilo Jeshi la Polisi Morogoro kupitia kwa RPC Mkoa Morogoro SACP. Alex Mkama limetoa wito kwa wananchi wote kuchukua tahadhari na kufuata maelekezo ya wataalamu wanapotembelea maeneo yenye upekee.

Chapisha Maoni

0 Maoni