Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Balozi, Dkt. Pindi Chana amezindua rasmi zoezi la Sensa ya
Wanyamapori ikiwa ni kuhesabu
Wanyamapori nchi nzima ili kuimarishs uhifadhi wa rasilimali za wanyamapori,
misitu ma kuendeleza utalii.
Akizungumza wakati wa uzinduzi sensa ya wanyamapori katika mfumo Ikolojia wa Nyerere - Selous -
Mikumi ambao ni mfumo mkubwa nchini wenye kilomita za mraba 104,143,
Waziri wa Maliasili
na Utalii, Balozi. Dkt. Pindi
Chana amesema Serikali imeendelea kuweka nguvu katika kuwahifadhi wanyamapori
nchini.
"Zoezi hili linathibitisha jitihada za Serikali ya
Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.
Dkt. Samia Suluhu Hassan katika uhifadhi wa rasilimali za wanyamapori na misitu
nchini na kuendeleza utalii," Mhe. Chana amesema.
Amesema Sensa hiyo katika ikolojia ya Nyerere - Selous-
Mikumi ni sensa ya 17 tangu kuanza
kuhesabu Wanyamapori katika eneo hilo ambapo sensa itafanyika kuanzia tarehe 5 Oktoba 2024 hadi Novemba 14,
2024.
Akizungumzia mchango wa
sekta hiyo kwa Taifa, Mhe. Chana amesema kupitia uhifadhi Sekta ya
Maliasili na Utalii inachangia asilimia 21% ya pato la Taifa, asilimia 25% ya
fedha za kigeni, kuzalisha ajira takribani milioni 1.6 za moja kwa moja na
zisizo za moja kwa moja.
Amefafanua kuwa Sensa hiyo itahusisha maeneo ya hifadhi za
Taifa za Nyerere, Mikumi, Mapori ya Akiba,
Selous, Lukwika-Lumesule, Liparamba na Jumuiya za Hifadhi za Wanyamapori
za Chingolie, Iluma , JUKUMU, Kisungule, Kimbanda, Mbaran'gandu,
NALIKA-Tunduru, Ngarambe-Tapika, Liwale na Maeneo ya wazi yanayozunguka mfumo
wa Ikolojia hiyo.
Naye, Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Utafiti wa Wanyamapori
Tanzania (TAWIRI), Dkt. Eblate Mjingo amesema sensa ya wanyamapori huonyesha
viashiria ambavyo ni changamoto kwa wanyamapori na huisaidia Serikali kutenga
rasilimali kwa ufanisi kukabiliana na ujangili, kuendeleza na kukuza utalii
pamoja na kupunguza migongano baina ya binadamu na wanyamapori.
Zoezi hilo linafanyika kwa ushirikiano wa Taasisi zilizo chini ya Wizara ya Maliasili na Utalii zikiwemo TANAPA na TAWA chini ya uratibu wa TAWIRI.
0 Maoni