Waziri Mkuu Kassim Majaliwa leo Oktoba 25, 2024 amewasili mkoani Kilimanjaro ambapo anamwakilisha Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika Maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Fimbo Nyeupe na Miaka 60 ya Chama cha Wasioona Tanzania (TLB).
Siki ya Kimataifa ya Fimbo Nyeupe
huadhimishwa kila Oktoba 15 kwa lengo la Kuelimisha jamii kuhusu haki na uwezo
wa watu wenye ulemavu wa kuona, Kutambua umuhimu wa fimbo nyeupe katika
kusaidia watu wenye ulemavu wa kuona kusafiri kwa usalama na uhuru na hatimaye
kufikia malengo yao.
Aidha, Siku hiyo pia ina lengo la
kuhamasisha ujumuishaji wa watu wenye ulemavu wa kuona katika jamii na
kuhakikisha wanapata fursa sawa katika elimu, ajira, na huduma zote nyingine.
Kaulimbiu ya maadhimisho hayo ni
“Upatikanaji wa Teknolojia Saidizi na Fikivu ni Mkombozi kwa Uchumi Endelevu
kwa Mtanzania asiyeona.”
0 Maoni