Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa
Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi amesema Mchezo wa makachu umekuwa
fursa nzuri ya kuitangaza Zanzibar
kimataifa .
Rais Dk. Mwinyi ameyasema hayo leo tarehe 24
Oktoba 2024 alipofika Bustani ya Forodhani Kuangalia Mchezo huo ambao umekuwa
maarufu na kuvutia wenyeji na wageni wengi wanaokuja nchini.
Aidha Rais Dk. Mwinyi amewasisitiza
Vijana wanaopiga makachu kuuendeleza Mchezo huo kwani umekuwa ukitizamwa na kufuatiliwa
na watu wengi sehemu mbalimbali kupitia mitandao ya kijamii.
Kwa upande wa Vijana wa makachu
walitumia fursa hiyo kumpongeza Rais Dk, Mwinyi kwa kuonesha mabango ya
mafanikio ya Serikali katika sekta mbali mbali.
Tukio hilo ni muendelezo wa shamra
shamra za kupongeza mafanikio ya miaka minne ya Serikali ya awamu ya nane chini
ya Uongozi wa Rais Dk. Mwinyi.
0 Maoni