TANAPA yadhamini Maonesho la Utalii na Uwekezaji Zanzibar

 

Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) ladhamini na kushiriki Maonesho ya Utalii na Uwekezaji Zanzibar 2024 (Zanzibar Tourism and Investment Show 2024) yanayofanyika Dimani- Fumba Visiwani Zanzibar.

Licha ya kuwa Mdhamini Mkuu wa Maonesho hiyo tumepata fursa ya kuungana na wadau wa Utalii, wawekezaji mbali mbali kutoka Zanzibar katika ufunguzi wa Maonesho hilo ambalo Mgeni Rasmi ni Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dkt. Hussein Ali Mwinyi, imesema taarifa ya TANAPA

Uwakilishi wa Shirika ulifanywa na Kamishna Msaidizi wa Uhifadhi na Maendeleo ya Biashara, Jully Lyimo (kwa niaba ya Kamishna wa Uhifadhi) ambapo alipata fursa ya kutoa neno la shukrani.

"Kama Shirika, tutaendelea kushirikiana na wadau wa Sekta ya Uhifadhi na Utalii katika kutangaza Utalii, fursa za Uwekezaji katika Hifadhi za Taifa Nchini pamoja na kutoa elimu ya Uhifadhi" amesema Lyimo.


Baadhi ya washiriki wa Maonesho ya Utalii na Uwekezaji Zanzibar 2024 (Zanzibar Tourism and Investment Show 2024) yanayofanyika Dimani- Fumba Visiwani Zanzibar, Oktoba 25-26 2024.

Chapisha Maoni

0 Maoni