Taarifa za
kisayansi zinazotokana na Mradi wa muda
mrefu wa Utafiti wa SIMBA SERENGETI
unaoratibiwa na Taasisi ya Utafiti wa Wanyamapori Tanzania (TAWIRI) kupitia Kituo cha Utafiti wa Wanyamapori Serengeti,
zimekua chachu katika uhifadhi na
kivutio cha Utalii ndani ya hifadhi ya
Taifa Serengeti.
Mradi huu wa
SIMBA SERENGETI unafuatilia idadi,
tabia na mienendo ya makundi ya simba kwa zaidi ya miaka 50, ambapo kwa sasa
yapo makundi 20 yenye jumla ya simba takribani 300 yanayofuatiliwa.
Aidha,
Katika mradi wa SIMBA SERENGETI utambulisho hufanyika kwa kila Simba kuandaliwa kadi maalumu (Lion
identification card) kwa kutumia
alama/madoa ya Kipekee kwenye uso eneo la ndevu (Whisker spots) na alama nyinginezo za asili.Utambulisho huu
husaidia kumfuatilia simba mmoja mmoja ndani ya kundi.
Aidha
matumizi ya teknolojia yanarahisisha utafiti wa simba ambapo kwa kutumia mikanda
ya simba yenye redio za mawasiliano (VHF/GPS satellite collars)
anayofungwa simba jike katika kila
kundi unasaidia kujua kundi lipo wapi.
Taarifa za
kisayansi za utafiti zinatoa dira
katika kuwahifadhi Simba, kunadi Utalii kupitia takwimu na
tabia za simba, ikikumbukwa Simba ni Miongoni mwa Wanyamapori wakubwa
ambao ni kivutio cha utalii (major tourism attraction) ambaye watalii wengi
wanapenda kumuona wanapokuja kwenye hifadhi.
#Tafiti za wanyamapori kwa ustawi wa uhifadhi na kukuza utalii nchini
0 Maoni