Rais Samia azungumza na wananchi wa Matemanga

 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza na wananchi wa Tarafa ya Matemanga, Wilaya ya Tunduru, aliposimama eneo hilo kuwasalimia, majira ya mchana, leo tarehe 26 Septemba 2024, akitokea Wilaya ya Namtumbo, ambako pia alipata fursa ya kusimama na kusalimia wananchi maeneo ya Likola, Rwinga na Mchomora.

Mhe. Rais Dkt. Samia ameingia wilayani Tunduru, akiendelea na ziara yake ya kikazi maeneo mbalimbali ya wilaya za Mkoa wa Ruvuma, ambayo anaitumia kupata mrejesho wa wananchi kuhusu mafanikio ya utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi ya 2020 - 2025, unaofanywa na Serikali ya CCM anayoiongoza, kupitia huduma na miradi mbalimbali ya maendeleo katika maeneo yao.

Aidha, Mhe. Rais Dkt. Samia anatumia ziara hiyo kusikiliza changamoto za wananchi na kuzichukua kwa ajili ya kuzifanyia kazi au kuzitolea maagizo ya ufumbuzi, kupitia mawaziri na watendaji wa Serikali aliombatana nao ziarani.






Chapisha Maoni

0 Maoni