Mkuu wa
Majeshi ya Ulinzi Tanzania, Jenerali Jacob John Mkunda amefanya Ziara ya Kikazi
nchini Msumbiji kuanzia tarehe 23 hadi 27 Septemba, 2024.
Wakati wa ziara hiyo, pamoja na masuala
mengine, Jenerali Mkunda alitembelea Ubalozi wa Tanzania uliopo Jijini Maputo
tarehe 24 Septemba, 2024 na tarehe 25 Septemba, 2024 alishiriki kwenye
Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Ulinzi la Msumbiji.
Wakati wa
Maadhimisho hayo, Jenerali Mkunda alitunukiwa na Mhe. Filipe Jancito Nyusi,
Rais wa Jamhuri ya Msumbiji, Nishani Maalum ya Heshima kwa kutambua na
kuheshimu mchango wa Tanzania katika ukombozi na ustawi wa amani na usalama
nchini Msumbiji.
Vilevile,
tarehe 26 Septemba 2024, Jenerali Mkunda alikutana na mwenyeji wake, Admiral
Joaquim Rivas Mangrasse, Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi ya Msumbiji na kuzungumza
masuala mbalimbali ya Ushirikiano kati ya JWTZ na Jeshi la Ulinzi la Msumbiji
(FADM) ambapo Viongozi hao walikubaliana na kusisitiza juu ya haja ya kuendelea kushirikiana kwa ukaribu
kwa maslahi ya nchi zetu mbili.
0 Maoni