Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Mhe. Mohamed Mchengerwa ametangaza kuwa uchaguzi wa Serikali za Mitaa utafanyika Novemba 27, 2024
Akitoa tangazo la Uchaguzi wa Serikali za Mitaa kwa mwaka
2024 leoa Jijini Dodoma, Waziri Mchengerwa amesema nafasi zinazowaniwa katika
uchaguzi huo ni pamoja na Wenyeviti wa Vijiji, Wajumbe wa Halmashauri ya
Vijiji, Wenyeviti wa Vitongoji, Wenyeviti wa Mitaa na Wajumbe wa Kamati za
Mitaa.
Mhe. Mchengerwa ameeleza kuwa ukomo kwa viongozi waliopo
sasa utakuwa ni Oktoba 28, 2024.
Waziri Mchengerwa ameongeza kuwa fomu za wagombea wa nafasi
hizo ambao ni kutoka vyama vya siasa vyenye usajili wa kudumu zitaanza kutolewa
Novemba Mosi hadi 07, 2024 na kampeni za uchaguzi zitaanza Novemba 20 hadi 26, 2024.
Kufuatia kutangazwa kwa tarehe ya kufanyika kwa uchaguzi huo wa Serikali za Mitaa, Waziri Mchengerwa amemuelekeza Mkurugenzi wa TAMISEMI kuhakikisha kuanzia Agosti 16, 2024 elimu ya upigaji kura inaanza kutolewa kwa wananchi ili waweze kufahamu namna ya kushiriki katika uchaguzi huo.
0 Maoni