Rais Samia atoa bilioni 7 uwanja wa ndege Arusha

 

Mkuu wa Mkoa wa Arusha Paul Makonda amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha Shilingi Bilioni 7 kuuboresha uwanja wa ndege wa Arusha katika jitihada za kuufanya uwanja huo kutoa huduma kwa saa 24.

"Mkandarasi ameshapatikana na mkataba umeshasainiwa na sasa hivi anamalizia usanifu na mkataba ni wa miezi 12 lakini jana tumekubaliana wamuharakishe kadri inavyowezekana angalau ndani ya miezi nane awe amemaliza kutufungia taa," alisema Makonda.

Kwasasa uwanja wa ndege wa Arusha unatoa huduma zake mchana pekee, suala ambalo limekuwa kikwazo kwenye jitihada za Rais Samia Suluhu Hassan za kukuza utalii wa Arusha na Tanzania kwa ujumla hasa wakati huu ambapo kunashuhudiwa wingi wa watalii wanaotokana na filamu ya kuvutia watalii kuja kutalii nchini Tanzania, filamu ya The Royal Tour.

Chapisha Maoni

0 Maoni