Wananchi wa tarafa ya Ngorongoro wilayani Ngorongoro wameendelea kuishi maisha magumu kutokana na kushambuliwa na wanyama wakali kufuatia matukio yanayoendelea kutokea katika eneo hilo.
Afisa tarafa wa eneo hilo bwana Bahati Mfungo amethibitisha kutokea
kwa matukio hayo na kusema kadri siku zinavyozidi kusonga mbele hali imekuwa ni
ya kutisha.
Katika matukio ya hivi
karibuni zaidi ya matukio mawili
yameripotiwa kutokea kwa wananchi na
mifugo kupoteza maisha au kujeruhiwa vibaya katika tarafa hiyo.
Mwananchi
anayejulikana kwa jina la Orkendenye Liarite mwenye umri wa miaka 32 kutoka kijiji cha Bulati akiwa machungani
alishambuliwa na simba ambapo alijeruhiwa vibaya huku ng’ombe wake wawili wakiuliwa na simba huyo.
Mwananchi huyo amejeruhiwa ubavu wa kulia na usoni na
kulazimika kukimbizwa haraka katika kituo cha afya cha Nainokanoka kwa ajili ya
matibabu.
Katika tukio lingine mwananchi anayeitwa Kimirei Kuya
mwenye umri wa miaka 26 alivamiwa na
kiboko ndani ya nyumba yake ambapo katika hali isiyo ya kawaida
alishambuliwa vibaya mwilini.
Tukio hilo limetokea katika kijiji cha Esere kata ya
Alaitole ambapo mwananchi huyo alivamiwa na mnyama huyo na kuuawa.
Kufuatia matukio haya serikali kupitia Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro (NCAA) inaendelea kutoa elimu, kuhamasisha, kuandikisha, kuthaminisha na kuhamisha wananchi ambao wanataka kuhama kwa hiyari ili kunusuru maisha ya watu hao.
0 Maoni